Picha: Mapenzi ya Chris Brown na Karrueche Tran yarudi kwa kishindo, ni baada ya kudaiwa kuachana
Bila shaka nuru ya mapenzi imerejea katika mioyo ya mwimbaji Chris Brown na model Karrueche Tran, baada Breezy kuthibitisha kuwa button ya uhusiano wao imerudi ‘on’.
Couple hiyo ya ‘On & Off’ imeonekana ikiwa na furaha baada ya Breezy kupost picha wakiwa pamoja kwenye mechi ya mpira huko L. A Jumapili (Agosti 17). Pamoja na kwamba Chris hakuweka caption yoyote lakini nyuso zao tu zinathibitisha kuwa wamerudiana.
Hivi karibuni Karrueche alidaiwa kumuacha Chris Brown, na miongoni mwa sababu zilizotajwa ni pamoja na kuwa Karrueche amekuwa hana furaha kutokana na Chris kufanya mambo yake kama mtoto, na pia kutumia muda wake mwingi kula bata badala ya kutengeneza muziki.
Vyanzo vingine vilidai kuwa Breezy ndiye aliyemuacha Tran na miongoni mwa sababu zilizotajwa ni kuwa amekasirishwa kwa kitendo cha Tran kuzungumzia uhusiano wao kwenye Interviews pamoja na Clothing Line yake, kwa lugha nyingine anaona kama anatumia mambo yao kupata attention imsaidie kibiashara (opportunist).