Alicia Keys, Usher, na Jay Z walivaa nguo za miaka ya 70! Kwenye sherehe ya kuzaliwa ya Beyonce aliyetimiza umri wa miaka 35.
Beyonce akiwa na ChancE The Rapper
Sherehe hiyo ilikuwa na mfanano wa Soul Train na kufanyika Jumatatu jioni.
Jay Z na Usher
Beyonce alitimiza umri wa miaka 35, Jumapili ya September 4. Akitoka kunyakua tuzo takriban 8 na kuvunja rekodi kwenye tuzo za MTV VMA, Beyoncé pia alichagua kusherehekea siku yake hiyo muhimu kwenye tamasha la mume wake la kila mwaka la Made in America huko Philadelphia.
https://www.youtube.com/watch?v=Q1t1-8QC7LI
Beyoncé alisafiriki hadi Camp David akiwa na mama yake, Tina Lawson, binti yake, Blue Ivy pamoja na Michelle, Malia, na Sasha Obama. Na baada ya kupongezwa na mastaa wenzake wakiwemo, Kim Kardashian, Mariah Carey, na Nicki Minaj, Beyoncé alielekea Philadelphia kujumuika kwenye tamasha hilo.
Diddy na mpenzi wake Cassie
Kwa mujibu wa CNN, Bey alikutana pia na rais wa zamani, Bill Clinton.
https://www.youtube.com/watch?v=3lHZIukox1A