Burudani
Rapper Wiista kuachia EP na album yake mwakani
Rapper Wiista ambaye zamani alikuwa msanii wa kundi la Navy Kenzo, amejipanga kuja na nguvu mpya mwakani.
“Wiista yupo studio akimalizia kurekodi EP yake atakayoiachia 2015 itakayofuatiwa na album mwishoni mwa mwaka,” imesema taarifa kutoka kwenye management yake, NGOMA Entertainment.
“Baada ya ukimya wa muda mrefu anarudi kwa kishindo na NAIYE na EP (Extendend Play), video itatoka katikati ya January.”
Mwaka huu, Wiista aliachia single yake mpya iitwayo ‘Naiye’. Unaweza kuusikiliza hapo chini.