Habari
RC atakayeniomba chakula, atakuwa anaomba kufukuzwa kazi – Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema Mkuu wa mkoa yoyote atakaye omba chakula kwake atakuwa ameomba kufukuzwa kazi.
Rais Magufuli ameyasema hayo leo, Mey 5, 2018 kwenye ufunguzi wa daraja la Kilombero, ambapo amesem akuwa haiwezekani mvua inyeshe halafu watu wakose chakula.
“Mkuu wa Mkoa atakayeniomba chakula, atakuwa anaomba kufukuzwa kazi, kwa sababu haiwezekani mvua inyeshe hivi, halafu wakose chakula,” amesema Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli amesema kuwa “maandiko yanasema asie fanya kazi na asile na asipo kula afe, hakuna chakula cha bure.”