
Kupitia kwenye kipindi chake cha RECAP & MANDO ameeleza kushangazwa na namna Msanii wa Nandy Yammi alivyoanza kiandaliwa Kiki kwa ajili ya muziki wake.
Anasema katika moja ya njia kubwa ya kumaliza kipaji chake na kuua muziki wake ni kupitia Kiki anazotengenezewa kwa sasa.
@el_mando_tz Anaongeza kuwa kwa sasa wasanii wengi hawataki kusainiwa kwenye lebo kutokana na aina ya uendeshaji wa lebo hizo.
Ametolea mfano lebo tatu ambazo ni The Afeican Princes, Konde Gang na Next Level , anasema katika lebo hizo wasanii wake wameshuka sana kimuziki ukilinganisha na namna maboss wao wanavyofanya muziki.
Anasema kuwa hiyo inaonyesha ni kwa namna gani hawakuwa tayari kuwa na lebo.
Ameuliza swali moja kwa mwaka 2023 wimbo gani wa Ibraah, Mac Voice na Yammi umetikisa kama ilivyokuwa zamani??
Unahisi kwanini wasanii wa lebo hizo wameshuka kimuziki hasa kwa takwimu??