RECAP: Rema auvaa ugomvi wa Kizz Daniel na Tekno (Video)
Bongofive Kupitia kipindi chake cha RECAP & MANDO el_mando_tz amezungumzia yanayoendelea mitandaoni kati ya Kizz Daniel na Tekno.
El_mando_tz anasema kwenye nyimbo ya Kizz Daniel & Tekno (Buga) ambayo ilitamba sana, kuna Blog moja ilinukuu taarifa kutoka kwa Tekno kuwa kwenye nyimbo hiyo ya Buga huwa kila mwezi analipwa na Kizz Daniel na hata akienda kufanya Show anamlipa Naira Milion 1, Tekno akajibu kwa kukanusha na kukataa kuwa Kizz Daniel hana uwezo wa Kumlipa Fedha hizo na kudai kuwa wimbo huo alifanya bila kulipwa chochote na wala Kizz Daniel hana Uwezo wa kunilipa hela hizo ndipo majibizano kati ya Tekno na Kizz Daniel yakaanza Rasmi.
Hii ilimfanya Msanii maarufu nchini Nigeria Rema kuingilia Ugomvi huo.
Kupata uchambuzi kamili tembelea ukurasa wa Bongofive Youtube:
Host: el_mando_tz
Cameraman: Samirkakaa
Imeandikwa na Mbanga B.