Burudani
Sad: Shaa ampoteza mama yake Mzazi
Muimbaji wa ‘Lava Lava’ Sarah Kaisi aka Shaa amefiwa na mama yake mzazi. Kwa muda mrefu Shaa alikuwa akimuuguza mama yake. Msiba upo nyumbani kwao Mikocheni, Dar es Salaam.
Shaa anakuwa msanii mwingine aliyefiwa na mama yake mwaka huu baada ya Barnaba, Z-Anto na Profesa Jay. Bongo5 inampa pole Shaa kwa msiba huo na Mungu ampe nguvu zaidi kwenye kipindi hiki kigumu.