Habari

Saudia: Vijana wapatiwa mamilioni ya pesa za kuoa

Mwanamfalme wa Saudia Muhammad Bin Salman ameidhinisha kutolewa kwa pesa milioni 3.74 za riyali, sawa na dola milioni 1 za kimarekani, ili zigawiwe kwa vijana 200 kama ruzuku ya kuoa.

Gazeti la serikali la Saudi Arabia limeripoti kwamba tangazo hilo lilitolewa na Shirika la habari la Saudia siku ya Jumapili.

Taarifa hiyo ilisema kuwa fedha hizo zitagawanywa kwa vijana wa kiume na wa kike kote nchini humo.

Limesema agizo la Mwanamfalme huyoni katika juhudi za kuwasaidia yatima wenye ulemavu na watu wenye ulemavu ambao wamekuwa na shida ya kuoa.

Katika awamu ya kwanza ya mpango huo, riyali milioni 250 za msaada zilisambazwa, kwa watu zaidi ya 26,000 kutoka maeneo tofauti ya nchi hiyo.

Licha ya kupewa pesa, vijana watafundishwa jinsi ya kutumia pesa.

Mpango wa Mwanamfalme Muhammed Bin Salman ulianzishwa kwa lengo la kuimarisha uchumi na jamii ya watu wa nchi hiyo kuboresha maisha ya watu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents