Habari

SHERIA: “Mwanaume atakayeoa mke mmoja atafungwa jela maisha” – King Mswati (III)

Mfalme wa Eswatini zamani (Swaziland), King Mswati III amewataka vijana nchini humo waliofikia umri wa kuoa, waoe haraka na kusisitiza kuwa wanatakiwa waoe wake wawili au zaidi, kinyume na hapo watafungwa.

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Mfalme imeeleza kuwa agizo hilo utekelezaji wake utaanza mwezi Juni, mwaka huu.

King Mswati III mpaka sasa ameoa wanawake 15 na ana watoto 25. Baba yake ambaye pia alikuwa mfalme wa nchi hiyo, alikuwa na wake 70 na watoto zaidi ya 150.

Imeelezwa kuwa takayekiuka agizo hilo atahukumiwa kifungo cha maisha jela.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa sababu ya agizo hilo ni kutokana na idadi kubwa ya wanawake nchini humo, inayopelekea ongezeko la watu kupungua.

Related Articles

Leave a Reply

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents