Burudani
Shilole afanya ‘maamuzi magumu’ kuhusu mpenzi wake Nuh Mziwanda baada ya sauti yake akimtongoza Wema Sepetu kuvuja
Baada ya sauti ya muimbaji wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda akimtongoza Wema Sepetu kuvuja, mpenzi wake Shilole ametoa msimamo wake juu ya penzi lao ambalo limekuwa likikumbwa na majanga kila mara.
Kupitia Instagram yake, Shishi ambaye ndiye alikuwa akionekana kuwa ‘victim’ wa tukio hilo kwa kusalitiwa na boyfriend wake, ameweka wazi msimamo wake juu ya penzi lao kwa kupost picha wakiwa pamoja na wenye furaha na kuandika “M siachani nawe na ntakupenda zaidi!”
Hata hivyo Nuh Mziwanda alikana sauti ile kuwa sio yeye ni ya kutengenezwa, na Shilole amemsamahe (Soma hapa).