Wachezaji wengi wazawa wakishafika Simba na Yanga wanahisi wamemaliza, kitu kinachopelekea kuwepo na ugumu wa kumpata Mshambuliaji Mzawa kariba ya John Bocco.
John Bocco ndani ya miaka 15 ya hivi karibuni amekuwa Mshambuliaji hatari zaidi kwa wachezaji wa Ndani na hii ni kutoka timu zote za NBC zikiwemo @simbasctanzania @yangasc na @azamfcofficial
Ana nidhamu, ana utulivu akiwa karibu na goli na licha ya umri wake, John Bocco akiwa uwanjani anakupa nafasi ya kuamini goli muda wowote linapatikana ukilinganisha na washambuliaji wengine wazawa tuliyonao kwenye Ligi Kuu.
Taja mshambuliaji mzawa mwenye uwezo wa kuvaa viatu vya John Bocco…?
Imeandikwa na @fumo255