Michezo

Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano hii, Madrid kuwapatia United, Gareth Bale na mkwanja juu ili kumng’oa Pual Pogba, Lacazette na wengine sokoni

Real Madrid wana mpango wa kumjumuisha mshambuliaji wa Wales Gareth Bale, 29, katika mkataba utakaowawezesha kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United na Ufaransa Paul Pogba, 26. (Mail)

Image result for bale and Pogba

United watalazimika kilipa zaidi ya pauni milioni £90 kumnunua beki wa Leicester City na England, Harry Maguire – hatua itakayomfanya kuwa nyota huyo wa miaka 26 kuwa mlizi ghali zaidi . (Telegraph)

United pia imetuma maombi ya kumnasa kiungo wa kati wa Uhispania na Dinamo Zagreb-Dani Olmo, 21. (Mail)

Mshambuliaji wa Arsenal na Ufaransa Alexandre Lacazette, 28, huenda akahama klabu hiyo msimu huu wa joto. (Express)Alexandre LacazetteAlexandre Lacazette(Kushoto)

Mlinzi wa Bournemouth na Uholanzi Nathan Ake, 24, huenda akatia saini mkataba wa kujiunga na Manchester City mhumu ujao. (L’Equipe, via Manchester Evening News)

Crystal Palace wanafanya kila juhudi kuhakikisha hawataiuzia Arsenal winga wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, na wana hasiri kwa sababu wanaamini Gunners wanafanya kusudi ili kumvuruga akili mchezaji huyo. (Mirror)Wilfried ZahaWilfried Zaha (Katikati)

Atletico Madrid wanataka kumsajili Lacazette kuchukua nafasi ya mshambuliaji Antoine Griezmann, 28 ambaye anaelekea Barcelona. (Mirror)

Winga wa Barcelona na Ufaransa Ousmane Dembele, 22, hana mpango wa kuondoka Nou Camp msimu huu wa joto licha ya vilabu vikubwa Ulaya ikiwa ni pamoja na Liverpool na Bayern Munich kuonesha nia ya kutaka kumsajili. (L’Equipe)

West Ham wanahofia huenda wakakosana na mshambulizi wa Austria Marko Arnautovic, 30, wasipomuuza. (Mirror)

Barcelona wako tayari kupokea maombi ya kumnunua mlinzi wa kati wa miaka 25-Mfaransa Samuel Umtiti, ambaye analengwa na Manchester United. (Sport, via Mirror)Samuel UmtitiUmtiti alijiungana Barcelona mwaka 2016

Chelsea wameafikiana kuhusu mkataba mpya wa muda mrefu na kiungo wa kati wa England Ruben Loftus-Cheek, 23. (Telegraph)

Mlizi wa Arsenal Mfaransa Laurent Koscielny, 33,ananyatiwa na Bordeaux. (L’Equipe)

Tetesi Bora Jumanne

Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, amekuwa akifanya mazoezi mjini New York licha ya wachezaji wenzake kurejea kambini kwa mazoezi ya kabla ya msimu mpya kuanza. (Sun)PogbaPogba

Barcelona wako tayari kulipa euro milioni 100 ya kumwezesha mshambuliaji wa Inter Milan Muargentina Lautaro Martinez, 21 kuondoka klabu hiyo kabla mkataba wake kukamilika. (Corriere dello Sport – in Italian)

Winga wa Manchester City Mjerumani Leroy Sane ameangaziwa katika uzinduzi wa jezi za msimu wa mwaka 2019-20, licha ya tetesi kuwa Bayern Munich wamekuwa wakimnyatia nyota huyo wa miaka 23. (Express)Leroy Sane

Arsenal wanashauriana na mshambuliaji wa Algeria, Yacine Brahimi 29 ambaye yuko huru na kujiunga na klabu nyinhine baada ya kuhama Porto. (Sky Sports)

Gunners pia wamepewa nafasi ya kusaini mshambuliaji wa Lyon na Ufaransa Nabil Fekir – kwa uero milioni 30. (Mirror)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents