Ukubwa wa muziki haupimwi kwa namna unavyochezwa redioni tena – Godzilla
Rapper Godzilla amesema kuwa kuna ngoma nyingi ambazo hazifanyi vizuri redioni lakini mtaani zinapendwa na kusikilizwa na watu kwenye simu zao.
Rapper huyo amedai kuwa redio sio kipimo tena cha muziki kufanya vizuri kwa sasa. “Watu wanazo nyimbo kwenye simu zao, wanadownload na kusikiliza,” Godzilla ameiambia Bongo5.
“Ukiuweka kwenye internet watu wanadownload na kuwa nazo, ndio muziki ulivyokuwa siku hizi. Ukitaka kujua hilo ni ukienda kwenye show, watu wanaimba na wewe,” ameongeza.
“Kwahiyo sasa hivi ukubwa wa muziki haupimwi ni kwa jinsi gani umesikika kwenye redio au kiasi gani cha rotation unapata, watu wanazo nyimbo kwenye simu zao. Muziki umekuwa mpana kwamba watu wanaweza kupata muziki kwa njia nyingi, kwenye internet, kutumiana kwenye whatsapp group kwahiyo watu wanazo tu.”