Burudani
Victoria Kimani atua Dar, atang’arisha uzinduzi wa The Playlist Ijumaa hii
Mwanamuziki na mrembo wa Kenya, Victoria Kimani, jana (March 5) alitua jijini Dar es Salaam akitokea Nairobi, Kenya.
Victoria alipokelewa na mtangazaji wa kipindi cha The Playlist cha Times FM, Omary Tambwe aka Lil Ommy. Kimani atahudhuria uzinduzi wa kipindi cha The Playlist, Ijumaa March 7, Club Infinity Mikocheni, nyuma ya Shoppers Plaza.
Mbali na muonekano maalum wa Victoria Kimani, kutakuwa na show kali kutoka kwa wasanii wa Tanzania, Linex, Navy Kenzo, Climax, Tunda Man, Dogo Janja, Wakazi na wengine wengi. Kiingilio ni 10,000/- tu.