Burudani

Video: Davido aelezea beef yake na Wizkid, ‘tuko poa lakini asiongee tena upuuzi juu yangu’

Hatimaye muimbaji wa Nigeria, Davido ameelezea beef inayoendelea kati yake na Wizkid na kudai kuwa hana tatizo naye lakini hakupenda vijembe alivyorushiwa na hitmaker huyo wa ‘Holla At Your Boy’.

“Kitu pekee kilichoniudhi ni kuhusu concert ya New York na tena nilikuwa nitweet kama ‘kila mmoja hakikisha ameenda kwenye show ya kaka yangu Wizkid’ na akanitupia vijembe kama hivyo. Siwezi kuvumilia hilo ndio maana niliamua kusema kama nilivyosema,” Davido aliiambia SaharaTV.

“Lakini yote poa tu mwisho wa siku inabidi kuendelea na muziki, shout outs kwake, bado mimi ni shabiki wake mkubwa, anafanya mambo yake. Hakukuwa na kitu lakini usinitupie vijembe, usifanye hivyo hasa kama ulipanda nami kwenye ndege moja,” aliongeza Davido akimaanisha kuwa siku hiyo hiyo walitoka kusafiri na ndege moja.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents