Michezo
Video: Goli la Rashford laipa kiburi Man United
Mfungaji wa goli la Man U,Marcus Rashford,
Klabu ya soka ya Manchester United usiku wa kuamkia leo imechomoza na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Celta Vigo katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya Euefa Europa Ligi.
Goli pekee la Man U limewekwa na mshambuliaji kinda anayekuja kwa kasi Marcus Rashford mnamo dakika ya 67 kipindi cha pili cha mchezo.
Manchester United yaibamiza Celta Vigo
Baada ya mchezo huo Timu hizo zitarejeana tena Alhamisi wiki ijayo katika Maskani ya Manchester United, Old Trafford.
BY HAMZA FUMO