Habari
Afrika Kusini: Jaji aliyetoa matamshi ya kibaguzi ajiuzulu
Jaji mwenye asili ya kizungu nchini Afrika Kusini, amejiuzulu baada ya kutoa matamshi ya kibaguzi mwaka jana, katika mitandao ya kijamii akisema kuwa matukio ya ubakaji ni utamaduni wa watu weusi.
Jaji huyo wa Mahama Kuu, Mabel Jansen, alikuwa katika mapumziko akisubiri upelelezi wa mahakama kufanyika juu ya sakata hilo. Matamshi hayo yalisemwa na rafiki yake ambaye hakutajwa jina.
Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi zenye asilimia kubwa ya matukio ya ubakaji duniani.
Na Emmy Mwaipopo
Chanzo: BBC