Habari

Video: Mwanamke atoa nguo na kubaki mtupu mbele ya sanamu ya hayati Nelson Mandela Afrika Kusini mchana kweupe!

Kisa cha mwanamke mmoja nchini Afrika Kusini aliyevua nguo zote na kubaki na suti yake ya kuzaliwa na kusimama mbele ya sanamu kubwa ya hayati Nelson Mandela, kimewaacha wapita njia na majirani waliokuwepo karibu na eneo hilo midomo wazi.

sa2

Kwa mujibu wa gazeti la Star, Jumatatu mchana ya wiki iliyopita mwanamke huyo ambaye hakufahamika alifika eneo la Sandton, Johannesburg ilipo sanamu hiyo akiwa amevaa vizuri. Ghafla akafanya kama ambavyo hufanya wakati wa kuoga, alitoa nguo zote na kusimama mbele ya sanamu hiyo na kuwapa watu onesho la bure huku wengine wakichukua picha na video exclusive za kupost katika mitandao ya kijamii.

Hata hivyo mwanamke huyo alipomaliza kufanya alichokuwa anakifanya (ambacho hakijulikani) alivaa nguo zake moja baada ya nyingine tena taratibu kama yuko chumbani kwake na kuondoka huku watu wakimshangaa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents