Burudani
Video: Vanessa Mdee na wasichana 25 wa Tanzania wajadiliana na Michelle Obama
Katika kuadhimisha siku ya msichana duniani (Oct 11), jarida la Glamour la Marekani, lilifanya majadiliano maalum yaliyopewa jina ‘Brighter Future: Global Conversation on Girls’ Education’ ambapo first lady wa nchi hiyo, Michelle Obama alizungumza na wasichana duniani kote kuhusiana na umuhimu wa elimu kwa mtoto wa kike.
Vanessa Mdee alikuwa pamoja na wanafunzi wa kike 25 wa Tanzania kwenye mjadala huo wao wakiwa kwenye ubalozi wa Marekani. Msichana aitwaye Nasra Abdallah alipata nafasi ya kumuuliza swali Michelle Obama.