Habari
Vijana tumieni kinga- Serikali yaonya, magonjwa ya ngono yaongezeka
Serikali imesema idadi ya watu wanaougua magonjwa ya ngono imeongezeka kutoka wagonjwa 458,914 hadi wagonjwa 480,448 mwaka huu.
Kutokana na hali hiyo Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa rai kwa Watanzania kutumia kinga ili kujikinga na magonjwa ya ngono.