Habari
Waendesha upatu wapigwa faini ya Sh Milioni 101 ama kwenda jela miaka 20 kwa makosa haya
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu wafanyabiashara wawili, Magdalena Uhwello na Halima Nsubuga kulipa faini ya Sh 101 milioni au kwenda jela miaka 20 baada ya kukiri kufanya biashara ya upatu na utakatishaji fedha.
Mahakama pia imetaifisha Dola za Marekani 124,433 zilizopo kwenye akaunti ya Equity Tanzania na Dola za Marekani 263,567 zilizopo kwenye akaunti ya Equity Uganda, fedha za wafanyabiashara hao, hivyo, jumla ya fedha ambazo zitaingizwa serikalini ni Shilingi bilioni moja.
Chanzo cha habari ni Azam Tv