Burudani
Wapo wanaotumia ndumba kwenye muziki lakini mimi… – Matonya
Msanii mkongwe wa muziki, Matonya amedai yeye haamini wala hatumii ndumba katika muziki wake.
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Sugua Benchi’ amedai wapo wasanii ambao wanatumia uchawi kwenye muziki.
“Wapo ambao wanaamini wakitumia panado wanapona kichwa, wapo wanaoamini wakitumia maji wanapona kichwa kalini pia wapo wanaoamini miti shamba,” alisema Matonya. “Kwa hiyo kwenye muziki wapo wanaotumia ndumba kufanikisha mambo yao lakini mimi sipo, mimi natumia uwezo wangu,”
Muimbaji huyo ambaye pia ni mkurugenzi wa Kundi la Black Image, amewataka mashabiki wa muziki kuendelea kuusuport wimbo mpya wa kundi hilo uitwao ‘Mr Legeza Kidogo’.