Burudani

Joh Makini: Lord Eyez bado ni msanii wa Weusi

Rapper kutoka kundi la Weusi, Joh Makini amevunja ukimya wa maneno yanayotembea mtaani yanayodai kuwa Lord Eyez amefukuzwa ndani ya kundi hilo.

14032973_680894472063312_21893298_n

Hitmaker huyo wa Perfect Combo amekiambia kipindi cha E News cha East Africa TV kuwa Eyez bado ni mmoja wa wasanii wa kundi hilo.

“Lord hajatengwa na bado ni mmoja wa wanafamilia katika kundi letu la Weusi kuna wimbo wa Lord tulikuwa studio tukiuandaa juzi. Watu wanaongea mengi kuhusu ukaribu wetu na Lord kwa sasa ila si mbaya wakituzungumzia kwa kuwa ni sehemu ya maisha yetu,” amesema Joh.

Kundi la Weusi linaundwa na wasanii watano akiwemo Joh makini, Nick wa Pili, G-Nako, Bonta na Lord Eyez.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents