Michezo
Yaya na Kolo Toure wafiwa na kaka yao wakati wakiendelea na kombe la dunia
Ndugu, Yaya na Kolo Toure wamepewa taarifa za kifo cha kaka yao Toure Oyala Ibrahim wakati timu yao ya Ivory Coast ikiendelea na kombe la dunia nchini Brazil.
Kaka wa wachezaji hao wa Manchester City na Liverpool amefariki jana akiwa na umri wa miaka 28 jijini Manchester kwa saratani ikiwa ni saa mbili baada ya Ivory Coast kufungwa mabao 2-1 na Colombia.
Chama cha soka cha Ivory Coast kimetoa pole kwa Yaya na Kolo imewataka wananchi kuwakumbuka katika sala wakati huu mgumu kwao.