Diamond Platnumz

Cocacola wamchukulia Diamond Platnumz ‘private jet’ kutoka Nairobi hadi Dar

Baada ya tukio la moto la leo kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta, JKIA jijini Nairobi, Kenya, lililosababisha uwanja huo kufungwa kwa muda na kumfanya Diamond Platnumz aliyetua alfajiri ya leo akitokea Afrika Kusini kukwamwa, Cocacola imemchukulia ndege binafsi itakayomleta Dar es Salaam.

Cocacola

Kupitia Instagram, Diamond ameshare picha wakati akipenda kwenye ndege hiyo ambamo atakuwa peke yake na rubani.

“Had no choice than dat, coz i miss my mum and Baby lyk crazy… @ Wilson Airport Nairobi… can’t wait to see you @rommyjones #I #MySelf #AloneInTheJet #CocaBoy …. #Cocacola Mmetisha sana, asanteni sana,” ameandika.

Diamond ni balozi wa Cocacola.

Hizi ni bei za kukodi ndege binafsi nchini Kenya.

Air Charter Rates at HKNW
Turbo-Props: $1,200 – $1,800/hr
Light Jets: $1,900 – $2,650/hr
Mid-size Jets: $2,700 – $3,400/hr
Large Jets: $3,600 – $7,800/hr

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents