Burudani

Kundi la Linkin Park la simamisha ziara yake

Ziara ya kundi la Linkin Park, imetangaza kusitisha kwa muda ziara yao iliyokuwa ikitarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwiki hii kutokana na kifo cha msanii mwenzao Chester Bennington.


Kundi la Linkin Park

Ziara hiyo imetajwa kufanyika wiki ijayo ila bado kauli rasmi haijatolewa, Kabla ya kifo cha msanii huyo kundi jilo la muziki lilitarajia kuangusha show kali maeneo ya Amerika Kaskazini ila kutokana na msiba walioupata wa kuondokewa na mwanamuziki mwenzao aliyefariki Alhamisi hii, wametangaza kusitisha ratiba zao ikiwemo ya upigaji picha jijini Hollywood.

Marehemu Chester(41), alifariki Alhamisi hii akiwa nyumbani kwake Palos Verdes Estates, mjini Los Angles, ameacha watoto sita na aliozaa na wanawake wawili tofauti.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents