Burudani
Kundi la Linkin Park la simamisha ziara yake
Ziara ya kundi la Linkin Park, imetangaza kusitisha kwa muda ziara yao iliyokuwa ikitarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwiki hii kutokana na kifo cha msanii mwenzao Chester Bennington.
Kundi la Linkin Park
Ziara hiyo imetajwa kufanyika wiki ijayo ila bado kauli rasmi haijatolewa, Kabla ya kifo cha msanii huyo kundi jilo la muziki lilitarajia kuangusha show kali maeneo ya Amerika Kaskazini ila kutokana na msiba walioupata wa kuondokewa na mwanamuziki mwenzao aliyefariki Alhamisi hii, wametangaza kusitisha ratiba zao ikiwemo ya upigaji picha jijini Hollywood.
Marehemu Chester(41), alifariki Alhamisi hii akiwa nyumbani kwake Palos Verdes Estates, mjini Los Angles, ameacha watoto sita na aliozaa na wanawake wawili tofauti.
Na Laila Sued