Afya

Madhara ya kujichua kwa wanawake na wanaume

Punyeto ni nini

Punyeto ni kitendo cha kufanya au kupiga punyeto, ni tendo la kutomasa sehemu zako mwenyewe za siri ili kujisisimua kimapenzi.

Haya ni baadhi ya madhara awezayopata mwanamke anayejichua au kufanya punyeto;

1. Inaharibu kizazi

2. Inakufanya kua mvivu mara kwa mara

3. Unakuwa unakosa hamu ya tendo

4. Maumivu ukeni yasiyo na sababu

5. Uke kuwa mlegevu yaani mtepeto

6. Hupelekea uke kutoa maji maji mara kwa mara au maji yale ambayo utoka kabla ya tendo kuto kuwepo ivyo itakufanya kupata michubuko na maumivu makali wakati wa tendo.

7. Uwezi kuja kujua raha ya tendo ukizoea punyeto sana wewe dada.

8. Punyeto inafanya uke wa mwanamke kukosa ladha kabisa hiyo itapelea kukimbiwa na mmeo au mwenzako kutafuta kamchepuko kenye uke mtamu.

9. Na ukizoea punyeto itakufanya kuwa mtu wa hasira hasira kila mara

10. Punyeto ni hatari kwa afya yako pia ukiizoea sana itapekekea kufanya mapenzi ya jinsia moja.

Hay ni baadhi ya madhara ya kupiga punyeto kwa wanaume

1. Punyeto hukufanya uwe dhaifu, inapoteza protini na kalsiamu ndani ya mwili wako.

2. Huleta matatizo kwenye neva nyurolojia ndani ya mwili.

3. Ni moja ya kisababishi kikuu cha uhanithi (uume kushindwa kusimama)

4. Ni rahisi kuwa mtumwa wa kujichua (teja) unaweza kujaribu mara 1 tu na tayari ukawa teja wa jambo hilo kila mara

5. Huleta uchomvu sugu na kwa haraka zaidi, mara nyingi utahitaji kulala usingizi hata nyakati za mchana

6. Husababisha mfadhaiko (stress) kwenye akili na kwenye roho yako pia

7. Huleta matatizo ya kisaikolojia, hukusababishia majonzi na huzuni na kukufanya kujilaumu nafsi mara baada ya kumaliza kujichua

8. Punyeto haifanyiki kirahisi, unahitaji akili yako iwaze au itazame picha mbaya au chafu au kumfikiria kimapenzi mtu asiyekuwepo hapo ulipo. Hili ni jambo baya zaidi kwa afya kwani picha hizo hazikuondoki haraka kichwani mwako tofauti na ukishiriki tendo la ndoa na binadamu mwenzio moja kwa moja.

9. Punyeto inakupelekea kufanya makutano haramu kwakuwa hiyo hamu yako ya kutaka kujichua kila mara itakupelekea kuanza kutafuta vijarida au picha za ngono jambo ambalo ni baya zaidi kwa afya yako ya mwili na roho

10. Punyeto inapelekea tatizo lingine kubwa zaidi nalo ni kuwahi kufika kileleni utakaposhiriki tendo la ndoa na mwenza wako, hii itakuletea shida kwenye mahusiano yako wewe mwenyewe na hata kwa mwenza wako.

11. Punyeto inapunguza uwingi wa mbegu (reduces your sperm count) kama matokeo yake mwanaume hataweza kumpa mwanamke ujauzito. Hili la kuwa na mbegu chache ndilo chanzo kikuu cha ugumba kwa wanaume na ni matokeo ya kupiga punyeto mara kwa mara.

12. Kimaadili kabisa punyeto au kujichua ni jambo baya, unamuwaza fulani na kujikuta ukishiriki tendo la ndoa peke yako. Hii inapunguza thamani yako na nidhamu kwa wengine. Unaweza kuwa mzuri kwenye maeneo mengine mengi lakini utaishia kuwa na matatizo kama hutaiacha tabia hii haraka.

Je ufanye nini ili kuacha punyeto au usishiriki mchezo huu mchafu?

Kama muda na umri haukuruhusu kuwa na mke au mchumba, basi fanya yafuatayo:

•Kama bado unasoma kuwa bize na masomo na ujiepushe na makundi hatarishi.

•Jishughulishe na mazoezi ya viungo kila siku. Hii itauchosha mwili wako na hivyo hutapata muda tena wa kujichosha zaidi kwa kujichua kwani tayari utakuwa na uwezo wa kupata usingizi mtulivu sababu ya mazoezi

•Usikae peke yako muda mrefu bila kuwa bize na shughuli yoyote. Kichwa kitupu ni nyumba ya maasi mengi.

•Epuka vyakula vyenye mafuta mengi

•Tumia muda ambao huna kazi kwa kulala na hivyo utakuwa unaipumzisha pia akili yako

•Usikae muda mrefu maeneo kama ya bafuni au chooni

•Usipende kujishikashika na mkono wako sehemu zako za siri wakati wowote.

•Futa picha zozote chafu iwe kwenye simu au computer yako na usitembelee blog au tovuti yoyote yenye picha hizo, kama upo kwenye magroup ya namna hiyo kwenye mitandao ya kijamii basi jiondowe haraka iwezekanavyo.

Chanzo.Dk Fadhili Paulo na Mitandao

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents