Bongo Movie

Mapenzi yapo moyoni sio machoni – Faiza

Muigizaji wa Filamu nchini, Faiza Ally amesema mapenzi yako moyoni sio machoni, huku akibainisha kuwa aliyekuwa baba watoto wake ‘Sugu’ bado anampenda ingawa watu wamekuwa wakizunguza mengi.

Kupitia mtandao wa instagram Faiza ameandika, “Yaani watu mnapenda kunitishia kuhusu Sugu, mngejua anavyonipenda huko aliko maisha tu. Mimi na Sasha ndio roho zake hata Mungu anajua msingekua mnaongea ongea, yaani ananipenda mpaka anakwepa kuniona anajifanya kama sipo lakin najua 24 hours niko kwenye akili yake.

“Sasha baba anatupenda sana na sisi tunajua halafu tukijua sisi inatosha, na anajua pia tunampenda sana, mapenzi yako moyoni sio machoni mwa watu!, sema tumechagua kuishi maisha yetu sio ya watu ndio inayo tukosti,” amemaliza kwa kuandiaka.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents