Picha

Mmarekani aliyemponda glasi ya bia Msomali ahukumiwa

Mmarekani aliyemponda na glasi ya bia mwanamke wa Kisomali kwakuwa alimsikia akizungumza Kiswahili, amepatikana na hatia.

20161017_102355
Jama akiongea na waandishi wa habari baada ya hukumu kutolewa

Tukio hilo lilitokea mwaka jana huko, Minnesota.

Jodie Marie Burchard-Risch alishtakiwa kwa kumshambulia Asma Jama, mhamiaji wa Kisomali kwenye mgahawa mmoja October 2015. Jama na familia yake walikuwa wamekaa kwenye mgahawa na walikuwa wakizungumza Kiswahili, lugha ambayo huizungumza wanapokuwa na watoto ili wasielewe baadhi ya vitu.

75d21a-forum01

Wakati kundi hilo likipita karibu na Burchard-Risch, aliwaambia “In America, we speak English.”

Jama alisema alipuuzia maneno hayo kabla ya mambo kuchemka zaidi pale Burchard-Risch alipomwambia kwa sauti kubwa arudi nchini mwake.
Baadaye Burchard-Risch alichukua glasi kubwa na kumpiga nayo usoni na kukimbia. Jama alijeruhiwa mdomo na alishonwa kwa nyuzi nyingi.

d6c81a-20151106-asmajama
Jama alishonwa nyuzi nyingi baada ya kujeruhiwa

Burchard-Risch amehukumiwa kifungo cha siku 180 jela na miaka mitano ya uangalizi. Pia atatakiwa kulipa fidia.

burchard-risch-jodie_1446750710689_443738_ver1-0
Jodie Marie Burchard-Risch

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents