Michezo
Mourinho asindikizwa na jeshi la polisi baada ya kutua Uingereza
Mourinho asindikizwa na jeshi la polisi baada ya kutua Uingereza
Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho pamoja na kikosi chake wamejikuta wakipata msaada wa jeshi la polisi baada ya kutua nchini Uingereza wakitokea kwenye ‘tour’ yao ya maandalizi ya msimu Marekani.
Mourinh anakuwa meneja pekee aliyebaki msimu huu Uingereza mabaye anapigiwa upatu kuondoka United kufuatia maendeleo yake kutoridhisha mashabiki wengi wa timu hiyo.
Vyombo vya habari vimeripoti kuwa mara baada ya meneja huyo kutua kwenye uwanja wa ndege wa Manchester wakitokea Marekani walipatiwa msaada wa polisi wa kuwasindikiza kwa kuhofia vurugu ambazo huenda zingefanywa na mashabiki wa timu hiyo.
Kwasasa United imerejea Uingereza kujiandaa na ligi kuu ya Uingereza huku ikionekana kutokuwa vizuri kwenye kikosi chake msimu huu.