Burudani

Mtoto mtarajiwa wa Kim Kardashian na Kanye West afahamika

Je unatamani kumfahamu mtoto anayetarajiwa kuzaliwa katika familia ya Kim Kardashian na mumewe Kanye West? Basi fahamu kuwa mtoto huyo atakuwa ni wakike kwa mujibu wa mtandao wa TMZ.

Mtandao huo umesema wawili hao wanatarajia kupata mtoto huyo kutoka kwa mwanamke ambaye wamemlipa kiasi kinachodaiwa kuwa ni dola 45,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 100 za kitanzania.

Wakati huo huo TMZ imeongeza kuwa, mwanamke huyo yupo chini ya uangalizi maalum wa madaktari ili kumsaidia mtoto atakaye zaliwa asipate madhara.

Endapo mtoto huyo atazaliwa atakuwa ni wa tatu katika familia Kim na Kanye baada ya North West na Saint West, lakini pia atakuwa ni mrembo wa tisa kwa familia ya Kardashian.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents