Bongo Movie

Muigizaji aliyejitokeza na kudai mtoto wa Mobetto ni wake ashambuliwa

Mshindi wa milioni 50 za Tanzania Movie Talent, Dennis Louis amesema mtoto wa Hamisa ni wake sio wa Diamond kama watu wanavyodai kauli ambayo imewafanya madau wengi katika mitandao ya kijamii kupingana na kauli hiyo huku wengine wakienda mbali zaidi kwa kudai kwamba ametumwa.

Muigizaji huyo amekuwa akipost vitu mbalimbali kupitia mtandao wake wa Instagram kujaribu kuthitisha kwamba mtoto huyo ni wake.

“Mengi yamesemwa nimevumilia vya kutosha mwenye mzigo nadhani mshanijua!! Kabla hamjaandika mambo zenu muwe na evidence za kutosha!!. Basi wenye wivu watasema Photoshop shubaaamit!!! #babajunior #comingsoon” amepost picha akiwa na Hamisa,” aliandika muigizaji huyo Instagram.

Katika post nyingine yenye picha yake na Hamisa Mobetto ameandika, “Siku tuliyomtengeneza junior wetu mimi na mama Dee pale magomeni usalama. Hotel siitaji..kila mtu apambane na huba lake…kuna mwenye tatizo huko!? Kama yupo kufwaaaz you know!!,”

Hata hivyo imebainika kuwa picha zote alizoweka Dennis akiwa na Hamisa sio halisi bali zinadaiwa kutengenezwa.

Mobetto hajaweka wazi mtoto wake huyo ni wa nani huku wadai wa mambo wakidai mtoto huyo ni wa Diamond.

Haya ni maoni ya mashabiki hao.

real_monie
Anatafuta kiki kwa pikipiki @angel_zadamz tumegomaaaa!!babake twamjua!

aronmwenga
Ila mbona mtoto anamdomo km wa yule jamaa..mnyama.?au karithi kwa babuyako?

Mdeecaroline
Mhhh…. We umejiedit kabisa na hyo suti yako nyeusi… Loooh.

stelambithe
Kumbe we do mwenye mimba..???????????????

naslike_
???? asanteee dadiii kwakuniletea mama mremboooo?? tho ulificha ila asante ????? @charles_willson

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents