Bongo Movie
Muigizaji wa filamu Haji Adam ahitimu stashahada ya Sanaa ya Maigizo, Bagamoyo
Mwigizaji wa filamu Haji Adam leo ametunikiwa Stashahada ya Sanaa ya Maigizo na filamu toka chuo cha sanaa Bagamoyo.
Katika mahafali yaliyofanyika kwenye ukumbi wa chuo hicho Haji pamoja na wahitimu wengine wamepata zawadi na vyeti mbalimbali toka kwa uongozi wa chuo hicho.
“Kwakweli nina furaha sana siku ya leo, namshukuru Mungu nimemaliza salama na natumai nikipumzika nitaendelea na masomo zaidi hapo mwakani,” Haji aliuambia mtandao wa Bongomovies.