Habari
Nas awekeza kwenye biashara ya viatu, kufungua duka lake soon!
Ni muda mrefu umepita bila kusikia kitu cha kumfanya Rapper Nasir bin Olu Dara Jones aka Nas azungumziwe sana kwenye mtandao, ukimya uliovunjwa kwa habari za duka lake jipya la sneekers analotegemea kufungua huko Las Vegas, Marekani.
Nas ambaye jina lake halijatokea katika orodha za mastaa wanamuziki wanaotengeneza pesa zaidi duniani, sasa ameonekana kuanza kuongeza vitega uchumi kwa fungua duka hilo la viatu.
Hivi karibuni Nasir alitweet picha yake akiwa site wakati ujenzi wa duka hilo alilolipa jina la “Sneaker Fiends” ukiwa unaendelea na kuandika “On the construction site for my sneaker store in Vegas !! Comin this year y’all. #SneakerFiends”.