Kundi la muziki la nchini Burundi, Best Life Music limekuja na video ya ngoma yake mpya, Overdose. Video ya ngoma hii ilifanyika Congo DR, Rwanda na Bujumbura (Burundi) na kuongozwa na Kent-P chini ya Kora Entertainment.
Kundi hili hufanya muziki kwa Kiingereza, Kiswahili, Kirundi na Kifaransa. Linaundwa na Young Dany, G Kiboko, Young Jpy and Mc Vitaa.