Michezo

Paulsen ataja Kikosi

Kocha mkuu  wa timu ya Taifa Star Jan Paulsen ametangaza kikosi cha timu hiyo itakayojulikana kwa jina la Kilimanjaro Star kitakachoshiriki michuano ya CECAFA Tusker  Cup 2010 inayotarajia kuanza tarehe  27 mwezi huu hadi Desemda 12,2010.

Kocha huyo alifungua dimba  kwa kutaja  majina  ya wachezaji kuwa ni Shaban Kado pamoja na Said Mhando na kipa Juma Kaseja.Wachezaji wengine ni shedrack Nsajigwa,Erasto Nyoni,Haruna Shamte,Stephano Mmasyika,Idrisa Rajabu na Juma Nyoso ambao ni mabeki.
Paulsen aliendelea kutaja viungo wengine  wakiwemo Shaaban Nditi,Henry Joseph, Nurdin Bakari,Jabiri Azizi,Niza Khalifan wengine ni Meshak Ab el,Mohamed Banka pamoja na Kigi Makisi.

Kocha huyu aliwataja washambuliaji kuwa ni pamoja na  Dan Mrwanda, Mrisho Ngasa, John Bocco,Thomas Ulimwengu na Gauence Mwaikimba , hivyo hawa ndio  watakaocheza  katika sakata hilo ambapo tayari nchi 12 , ikiwemo Tanzania , Kenya, burundi, Uganda,Rwanda, Somalia,Ethiopia, Sudan, Zanzibar na timu nyingine zilizokaribishwa ni kutoka  Ivory Cost, Zambia pamoja na Malawi.

Awali Brand Meneja Breweries LTD(SBL) Tusker, Nandi Mwiyobella slisema,  ’Tumeahidi kupanda kwa viwango vya wachezaji wa  timu Afrika ya Mashariki na Kati, ili kuwawezesha hata kushiriki katika mashindano ya Kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazili na kusema, chapa ya Tusker  ina moyo huo.
Nandi aliendea kusisitizia kuwa wakiwa kama wadhamini wakuu wa michuano ya CECAFA watahakikisha Tanzania inaweka historia na kufanya vizuri kwani wamejipanga vizuri kwenye  michuano ya CECAFA.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents