Uncategorized
Rais Magufuli akabidhiwa ramani ya uwanja mpya wa soka utakaojengwa Dodoma (+video)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na wataalamu wa ujenzi wa uwanja wa soka unaotarajiwa kujengwa Jijini Dodoma na kukabidhiwa ramani ya uwanja wa kisasa wa mpira utakaojengwa jijini Dodoma.
Mazungumzo hayo pia yalihudhuriwa na wataalam wa ujenzi wa uwanja kutoka Morocco na pamoja na Balozi wa Morocco nchini Tanzania, Abdelillah Benry.
Uwanja huo unatarajia kujengwa eneo la Nara Jijini Dodoma, barabara ya kuelekea Singida ambapo jumla ya hekari 143 zimetengwa. Unatarajia kugharimu Tsh bilioni 56 na ukiwa na uwezo wa kubeba watazamaji 85,000.