Michezo
Zlatan apewa likizo ya siku 4 na Jose Mourinho
Kocha wa Manchester United Jose Mourinho ametoa likizo ya siku 2 kwa wachezaji ambao hawajaitwa timu ya Taifa, ila mshambuliaji Zlatan pekee amepewa likizo ya siku 4.
“Katika umri wa miaka 34,unahitaji kupumzika. Amecheza kila mechi, kila dakika siku 4 za mapumziko kwake,” amesema Jose.
Mchezaji huyo raia wa Sweden ameshafunga magoli manne kwenye mechi zake nne za kwanza akiwa na United.