Habari
Rwandair kushusha ndege mbili mwishoni wa mwaka huu
Shirika la ndege Rwanda (Rwandair), linatarajia kuingiza ndege zake mbili mpya aina ya Airbus A330 zenye uwezo wa kubeba abiria 276.
Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es salaam, meneja mkazi wa shirika hilo nchini, Ibrahim Bukenya amesema, “ndege hizo zitaanza safari zake kuanzia mji wa Bombay nchini India na Guanghazou nchini China zikitokea Kigali Rwanda.”
Alimalizia kwa kusema ndege hizo zitawasili kabla ya mwisho wa mwaka huu.
BY: EMMY MWAIPOPO