Burudani
Mtoto wa Chris Brown sasa ni Royalty Brown rasmi
Chris Brown na mzazi mwenzie, Nia Guzman wamemaliza vita vyao kuhusiana na haki ya kila mmoja kukaa na mtoto wao pamoja na jina lake rasmi kwenye cheti cha kuzaliwa.
Vyanzo vimeuambia mtandao wa TMZ kuwa Chris na Nia wamekubaliana rasmi kumlea pamoja mtoto huyo. Chris atakaa naye kwa siku 12 katika mwezi na hakutakuwa na usimamizi.
Kuhusiana na jina la mtoto wamekubaliana kuwa ataitwa Royalty Brown bila jina la katikati.
Chris atakuwa akimlipa Nia $2,500 kwa mwezi. Pia atakuwa akimlipa dola 15,000 kwa mwezi kama ‘back support.’
Chris pia atakuwa akimsomesha Royalty, kulipia matibabu yake na bima ya afya na gharama za walezi.