Burudani
Picha: Davido ashoot video ya wimbo wake mpya
Davido bado ana hasira ya kukaa takribani mwaka mmoja bila ya kuachia video wala nyimbo yeyote. Muimbaji huyo amekamilisha kutengeneza video yake nyingine ambayo inadaiwa itatoka muda si mrefu.
Video hiyo ambayo inadaiwa kufanyika nchini Afrika Kusini. Davido amemtumia mwanamitindo maarufu wa nchini humo ambaye amezaliwa nchini Uingereza, Nqobilé Ntshangase ambaye katika mtandao wa Instagram anatumia jina la @nqobiledanseur.
Kupitia mtandao wa Twitter, Nqobilé amethibitisha kuwa video hiyo itatoka muda si mrefu kwa kuandika, “@iam_Davido #IF ???? SOON COME!!!! ????????x????????.” Tazama picha zaidi hapa chini.