Habari
Adama Barrow achaguliwa kuwa Rais mpya wa Gambia
Aliyekuwa mgombea wa chama cha upinzani kwenye uchaguzi mkuu wa nchini Gambia, Adama Barrow amechaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo.
Mgombea huyo amemshinda aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh aliyeongoza Gambia kwa miaka zaidi ya 20.
Akitangaza matokeo hayo Ijumaa hii mkuu wa tume ya uchaguzi alimtangaza Barrow kushinda kwa kura 263,515 dhidi ya 212,099 alizozipata Rais Yahya.