Meneja wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Simba SC, Ahmed Ally amempongeza Ally Kamwe kupata nafasi ya kuwa Afisa Habari mpya kwa watani zao Yanga SC.
Akizungumza na Wasafi fm pamoja na kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram, Ahmed Ally amesema kuwa amemmiminia pongezi hizo Ally Kamwe huku akitupa dongo kizani kwa kudai kuwa hapo awali walikuwa na mamluki. ”Kwa siku za hivi karibuni walikuwa wana haha, ikafika muda wakachukua hadi mamluki kuja kuwafanyia kazi.”