Burudani

Bob Marley atimiza miaka 40 tangu afariki Dunia

Ni miaka 40 tangu mwimbaji mashuhuri wa rege Bob Marley alipokufa na saratani huko Miami, akiwa na umri wa miaka 36, ​​mnamo 11 Mei 1981.

Bob Marley seen in London in 1977

Bob Marley akiwa London mwaka 1977

Mwanamuziki huyo ni mmoja wa wasanii mashuhuri na wanaotambulika katika historia ya muziki, na vibao vikiwemo No Woman No Cry, One Love, na Redemption Song.Bob Marley performs on stage in the Netherlands

Bob Marley anatumbuiza huko Houtrust Hallen huko The Hague, Uholanzi, mnamo 1977 (hapo juu na chini

Kibao chake cha Buffalo Soldier kilikuwa kikubwa zaidi nchini Uingereza, na kufikia nambari nne mnamo Mei 1983.

Albamu ya 1977 Exodus iliitwa Albamu ya Karne na Jarida la Time.Bob Marley performing on stage in the US in 1979

Bob Marley akitumbuiza Marekani mwaka wa 1979

Marley alizaliwa mnamo 1945 kwa baba mzungu wa tabaka la kati na mama mweusi, huko Jamaica.

Utotoni mwake kulikuwa na umasikini na hakuwa akiwasiliana na baba yake, afisa wa jeshi la majini ambaye alifanya kazi katika serikali ya Uingereza.

Aliondoka nyumbani akiwa na umri wa miaka 14 na kuendelea na kazi ya muziki huko Kingston.

Mnamo 1972, Marley aliwasili Uingereza na bendi yake ya The Wailers kufanya ziara na Johnny Nash kwa matumaini ya kuzindua taaluma yake ya kimataifa.Bob Marley and The Wailers pose on steps in London

The Wailers (Earl Lindo, Aston Barrett, Bob Marley, Peter Tosh, Carlton Barrett na Bunny Wailer) wanapiga picha mnamo 1973 huko London

Mwaka uliofuata, Wailers walitoa albamu yao ya Catch a Fire na wakaanza kucheza kwenye televisheni ,BBC.

Uonekano huo ulileta athari kubwa na ukawapa hadhira pana nje ya msingi wa mashabiki wao wa jadi.Bob Marley and the I-Threes perform together at the Rainbow Theatre in London in 1977

Bob Marley na I-Threes (Judy Mowatt, Rita Marley na Marcia Griffiths) wakicheza pamoja katika ukumbi wa Rainbow Theatre huko London mnamo 1977

Bob Marley plays at a hotel in London in 1978

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,Bob Marley akitumbuiza katika hoteli London mwaka 1978

Baada ya ziara nyingine mnamo 1975, rekodi ya No Woman No Cry ya moja kwa moja huko The Lyceum, London, ilitolewa kama wimbo mmoja na ikampa Marley kibao chake cha kwanza Uingereza.

Mwimbaji huyo aalijikita katika muziki na akawa jina la kutambulika

Bob Marley performs at the West Coast Rock Show at Ninian Park in Cardiff, Wales, in 1976

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,Bob Marley anatumbuiza kwenye Maonyesho ya West Coast Rock huko Ninian Park , Cardiff, mnamo 1976 (juu na chini)Bob

Bob Marley performs at the West Coast Rock Show at Ninian Park in Cardiff, Wales, in 1976

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Marley alikuwa anajulikana kwa imani yake ya Rastafarian, pamoja na mkewe, Rita, na dini hiyo ilionekana katika muziki wake.

Bob Marley sits at a table holding a pen

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,Bob Marley alionekana mnamo 1979 huko Hollywood Tower Records, California, Marekani

Mwimbaji huyo pia alikuwa akipenda sana mpira wa miguu na alijulikana kwa kukaragaza ngozi kati ya vikao vya studio au kabla ya kupanda jukwaani.

Bob Marley on a football field in Rio de Janeiro, Brazil, in 1980 with football player Paolo Cesar Caju and singer-songwriter Chico Buarque

CHANZO CHA PICHA,ALAMY

Maelezo ya picha,Bob Marley (katikati) akiwa na mchezaji wa mpira Paolo Cesar Caju (kushoto) na mtunzi wa nyimbo Chico Buarque (kulia) kwenye uwanja wa mpira huko Rio de Janeiro, Brazil, mnamo 1980

“Ninapenda muziki kabla ya kupenda mpira wa miguu,” alisema kwenye mahojiano mnamo 1980.

“Kucheza mpira wa miguu na kuimba ni hatari kwa sababu mpira una vurugu sana. Ninaimba juu ya amani, upendo na vitu vyote hivyo, na kitu kinaweza kutokea.

“Mtu akikukabili kwa mabavu huleta hisia za vita.”

Onyesho la mwisho la moja kwa moja la Marley nchini Uingereza lilikuwa mnamo 13 Julai 1980 huko New Bingley Hall, Stafford.

Marley alikufa mwaka uliofuata kwa sababu ya ugonjwa wa melanoma ya acral lentiginous, baada ya kugunduliwa kuwa nao mnamo 1977. Alizikwa mahali pake pa kuzaliwa Jamaica katika kijiji cha Nine Mile.

Bob Marley seen in 1978

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,Bob Marley mwaka wa 1978

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents