Michezo
Bondia wa kwanza kuvaa Hijab Olimpiki 2024
Kutana na Mwanadada Bondia wa kwanza wa Australia kuvaa Hijab kwenye mashindano ya Olimpiki toka yalivyoanzishwa mashindano hayo anajulikana kwa jina la Tina Rahimi.
Anaandika historia kwa kuiwakilisha Australia katika michezo ya Olimpiki akiwa amevaa Hijab, Bondia huyo alizaliwa na wazazi wenye asili ya Iran na alianza kama msanii wa Vipodozi kabla ya kuingia katika masumbwi kama mchezo wa kujifurahisha lakini sasa anajiandaa kuwakilisha Nchi yake huko Paris.