Burudani

Bushoke azungumzia project yake inayofata baada ya uchaguzi

Ruta Maxmillian Bushoke ni miongoni mwa wasanii waliokuwa busy na show za kampeni zilizodumu kwa miezi miwili.

Bushoke

Kutokana na kutingwa na show hizo, Bushoke alilazimika kusubiri hadi mambo ya uchaguzi yamalizike ili aweze kurejea kikamilifu kwenye muziki.

Bushoke ameiambia Bongo5 kuwa baada ya uchaguzi kumalizika hivi sasa anajipanga kushoot video ya wimbo wake ‘Angel’ aliowashirikisha Mr Blue pamoja na Dullysykes ambao ulitoka mwezi March mwaka huu. Video hiyo itaongozwa na director Eddie Juma.

Kuhusu project mpya, Bushoke amesema kuna wimbo mpya ambao anatarajia kuurekodi siku si nyingi ambao ndio utakuwa official single ambayo hakupenda kuizungumzia zaidi mpaka pale mambo yatakapokaribia kukamilika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents