Michezo

Cameroon waomba msaada FIFA baada ya wachezaji wake kugoma

Timu ya taifa ya Cameroon imekumbwa na mgomo wa wachezaji wake saba, ambao wamesema hawataki kwenda kushiriki michuano ya kombe la mataifa ya Afrika itayoanza hivi karibuni kuanzia Januari 14 mwakani huko nchini Gabon.

Wachezaji hao saba wasiotaka kuwa sehemu ya kikosi ni pamoja na beki mahiri wa Liverpool Joel Matip, ambae haijaichezea timu hiyo ya taifa toka mwaka 2014.

Kocha wa kikosi cha Cameroon Hugo Broos, amesema wachezaji wameweka maslahi yao binafsi juu ya yale ya timu ya taifa hivyo shirikisho la soka la nchi hiyo linatakiwa kuchukua hatua kwa wachezaji hao kwa mujibu wa kanuni za Fifa

Allan Nyom, anayechezea timu ya West Bromwich Albion, amemwambia kocha Broos, anataka kubaki kuendelea kuitumia klabu yake ili kulinda nafasi yake katika timu hiyo inayoshiriki ligi kuu England.

Wachezaji wengine wasiotaka kujuishwa kwenye timu hiyo ni Andre Onana wa Ajax Amsterdam, Guy N’dy Assembe wa Nancy, Maxime Poundje anayechezea Girondins Bordeaux ,Andre-Frank Zambo Anguissa wa Olympique Marseille pamoja na Ibrahim Amadou anayekipiga na Lille

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents