Michezo
Campbell atua Dar kwa kishindo atembelea timu ya walemavu (Video+Picha)
Beki wa zamani wa klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Uingereza, So Campbell ametembelea timu ya walemavu ya Muungango mara baada ya kutua nchini hii leo.
Campbell yupo nchini hivi sasa kwa ziara ambayo ni mualiko wa Kampuni ya kubashiri matokeo (Sportpesa) Tanzania, amepata nafasi ya kufanya mazungumzo na wachezaji wenye ulemavu wa viungo pamoja na viongozi wa kamati ya michezo ya watu wenye ulemavu Tanzania Paralympic Committee(TPC) katika viwanja vya karume Jijini Dar es salaam na kisha kugawa Jezi kwa timu hizo.
Picha za matukio ya So Campbell alipo wasili Uwanja wa Karume TFF na namna alivyoshiriki na timu ya walemavu ya Muungango
By Hamza Fumo