Burudani
Darassa kuja na mradi wa ‘Magic Muziki’
Rapper Darassa amesema ameamua kuanzisha kundi la muziki liitwalo ‘Magic Muziki’ litakalokuwa likiunganisha wasanii wachanga na ambao atakuwa akiwasaidia kimuziki.
Darassa amesema ameamua kuanzisha kundi hilo ili aweze kuwasaidia wasanii hao kwa pamoja.
“Tayari kuna project kadhaa nimesharekodi, ngoma nimetunga mimi, nimewapeleka studio madogo na mpaka sasa kazi ipo safi. Hawa wasanii watakuwa wanaitwa Magic Muziki, ni kama kundi fulani. Kwahiyo watu wategemee baada ya kumaliza kazi zangu nadhani mwezi wa kumi na moja kazi zao zitaanza kusikika,” amesema.