Michezo
David Moyes kocha mpya West Ham United
Klabu ya West Ham inatarajia kumthibitisha David Moyes hapo kesho siku ya Jumanne kuwa meneja mpya wa timu hiyo akichukua nafasi ya Slaven Bilic aliyeachishwa kazi leo.
Moyes ambaye aliwahi kuifundisha Manchester United na Everton atakuwa kocha wa 16 ndani ya klabu ya West Ham huku akitarajiwa kusaini mkataba wa kuitumikia timu hiyo kwa miezi sita.
West Ham yamtimua kazi kocha wake Slaven Bilic
Kibarua cha kwanza cha Moyes kitakuwa siku ya Jumapili ya Novemba 19 atakapo ikabili Watford huko Vicarage Road.